VIJANA WATAKIWA KUACHA UTAZAMAJI, WACHANGAMKIE MIKOPO YA SERIKALI KUJIKOMBOA KIUCHUMI


Na Suzy Butondo,Shinyanga

Vijana wametakiwa kuacha kuwa watazamaji wa fursa mbalimbali zinazotolewa na serikali badala yake watumie fursa hiyo kuwekeza kupitia fedha za mkopo zinazotolewa na serikali kuanzisha miradi itakayowakwamua kiuchumi.

Rai hiyo imetolewa na Waziri wa nchi Ofisi ya Rais maendeleo ya vijana Dkt. Joel  Nanauka  wakati wa uzinduzi wa Jukwaa la vijana Mkoa wa Shinyanga,ambapo  amewataka vijana kuwekeza kwenye muda na kuchangamkia fursa bila kusubiri kuonewa huruma.

 Amesema kufanikiwa kunatokana na ndoto ulizonazo,ikiwa ni pamoja na kuwa na nidhamu  ya muda hatua ambayo itawafikisha kwenye mafanikio badala ya kuendelea kulalamika bila kuchukuwa hatua ili kuondokana na umasikini.

“ Vijana tumieni  fursa kupitia fedha zilizotolewa na serikali Sh 200 bilioni kuandika maandiko ya miradi ambayo italenga kuanzisha jambo ambalo litaleta tija na kuweza kuwasaidia vijana”amesema Nanauka.

Amesema serikali imeondoa masharti magumu yaliyokuwa kikwazo kwa vijana kunufaika na mikopo, likiwamo sharti la dhamana isiyohamishika, ili kuwawezesha vijana wengi zaidi kupata fedha za uwezeshaji Sh bilioni 200 zilizotolewa na Rais Samia Suluhu Hassan kupitia Ofisi ya Rais, Maendeleo ya Vijana.

Nanauka amesema masharti yaliyokuwa yanawakwamisha vijana wengi kupata mikopo sasa yamefutwa, ikiwamo dhamana isiyohamishika, huku marejesho yakianza kati ya miezi mitatu hadi sita baada ya kupokea mkopo, ili kuwapa muda wa kukuza miradi yao.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Maendeleo ya Vijana, Joel Nanauka akizungumza na vijana mkoani Shinyanga wakati akizundua Jukwaa la Vijana mkoani humo.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Maendeleo ya Vijana, Joel Nanauka akizungumza na vijana mkoani Shinyanga wakati akizundua Jukwaa la Vijana mkoani humo.
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mboni Mhita akizungumza kwenye uzinduzi wa Jukwaa la Vijana mkoani humo.
Katibu Tawala wa Mkoa wa Shinyanga CP Salum Hamduni akizungumza.





Post a Comment